Thursday, July 30, 2026

Nairobi 97.7 Western 89.3 Eldoret 92.3 Kitui 105.6 Taita 94.9 North Rift 84.7 Kibwezi 87.9

VIONGOZI WA SERIKALI WAMRAI KALONZO KUJIUNGA NA SERIKALI

Baadhi ya viongozi wa muungano wa Kenya Kwanza wamemtaka kiongozi wa chama cha Wiper Democratic Movement Kalonzo Musyoka kujiunga na serikali.

Viongozi hao wamesema ushirikiano wa kisiasa unaweza kusaidia kuimarisha umoja wa kitaifa na kuharakisha utekelezaji wa ajenda za maendeleo nchini.

Hata hivyo, Kalonzo ameendelea kusisitiza msimamo wake wa kuendelea kuwa upande wa upinzani, akisema atashirikiana na viongozi wengine wa muungano wa upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Imetayarishwa na Hilda Ajema

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *