HARRY KANE AZAMISHA DR CONGO
England imefuzu hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia baada ya kugeuza matokeo na kuichapa DR Congo mabao 2-1, huku nahodha Harry Kane akifunga mabao yote mawili ya ushindi.
DR Congo ilikuwa mbele kupitia bao la Brian Cipenga, na ilionekana kuelekea kuiondoa England kabla ya Kane kusawazisha dakika ya 75 kwa kichwa na baadaye kufunga bao la ushindi dakika ya 86.
Ushindi huo umeinusuru England dhidi ya moja ya fedheha kubwa katika historia yake ya Kombe la Dunia na kuihakikishia nafasi katika hatua ya 16 bora ya mashindano hayo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

