MASHINDANO YA SHULE ZA UPILI NGAZI ZA MKOA KUENDELEA WIKI HII
Mashindano ya muhula wa pili ya Shule za Sekondari Kenya (KSSSA) Yameanza katika mikoa kadhaa yakiwakutanisha wanafunzi kutoka shule mbalimbali nchini kuwania ubingwa katika michezo tofauti.
Mashindano yataanza kwa ngazi za mikoa katika maeneo yote nane ya nchi kabla ya fainali za kitaifa zitakazofanyika katika MPESA Academy kuanzia Julai 28 hadi Agosti Mosi.
Wakati huo huo, Benki ya KCB imetenga shilingi milioni 20 kudhamini mashindano hayo, fedha zitakazotumika kununua vifaa vya michezo, zawadi na kuendesha shughuli mbalimbali za mashindano.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

