Thursday, July 30, 2026

Nairobi 97.7 Western 89.3 Eldoret 92.3 Kitui 105.6 Taita 94.9 North Rift 84.7 Kibwezi 87.9

SERIKALI YAHAKIKISHIA WAKENYA UPATIKANAJI WA MAFUTA

Serikali imewahakikishia Wakenya kuwa upatikanaji wa mafuta nchini unaendelea kuwa wa kutosha licha ya mvutano unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.

Katika taarifa yake, Waziri wa Nishati na Petroli Opiyo Wandayi amesema hali ya usafirishaji wa mafuta duniani imeathiriwa na mzozo unaozunguka Mlango wa Hormuz, lakini usambazaji wa mafuta nchini Kenya haujakatizwa.

Wandayi amesema shehena zote za mafuta zimeendelea kuwasili kwa wakati kupitia mpango wa serikali wa uagizaji wa mafuta kati ya serikali na serikali (G2G), hatua ambayo imechangia kudumisha utulivu wa bei na upatikanaji wa mafuta nchini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *