Thursday, July 30, 2026

Nairobi 97.7 Western 89.3 Eldoret 92.3 Kitui 105.6 Taita 94.9 North Rift 84.7 Kibwezi 87.9

WAMATANGI APINGA WITO WA KUGAWA KAUNTI YA KIAMBU

Gavana wa Kaunti ya Kiambu, Kimani Wamatangi, amepinga wito wa baadhi ya viongozi wa kisiasa wa kutaka Kaunti ya Kiambu itenganishwe na eneo la Mlima Kenya au igawanywe kuwa kaunti mbili.

Wamatangi amesema mapendekezo hayo yana nia ya kisiasa na yanalenga kuleta mgawanyiko badala ya kuendeleza maslahi ya wananchi.

Aidha, amewataka viongozi wanaounga mkono mpango huo kueleza maendeleo waliyoyatekeleza walipokuwa madarakani, akisisitiza kuwa wakazi wa Kiambu wanahitaji huduma na maendeleo, si siasa za migawanyiko.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *