MAANZO AWAHIMIZA WAPIGAKURA WA OL KALOU KUDUMISHA AMANI
Seneta wa Makueni, Dan Maanzo, amewataka wapigakura wa Ol Kalou kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mdogo wa ubunge bila hofu wala vitisho.
Maanzo amesema wananchi wanapaswa kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura kwa amani na bila kushawishiwa au kutishwa na mtu yeyote.
Aidha, amewahimiza kuripoti mara moja kwa mamlaka husika jaribio lolote la kuzua vurugu au kuvuruga mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na uwazi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

