MATIANG’I AONYA KUHUSU USALAMA WA TAIFA KISA ONGEZEKO LA WAHUNI
Aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Dkt. Fred Matiang’i, ameonya kuwa Kenya inaelekea katika hali ya machafuko kutokana na kuongezeka kwa vurugu za kisiasa, visa vya utekaji nyara na matumizi ya makundi yenye silaha kuwashambulia wakosoaji wa serikali.
Matiang’i amelaani tukio la Keumbu, Kisii, ambapo washiriki wa mkutano wa kisiasa walirushiwa mawe mbele ya maafisa wa polisi waliokuwa eneo hilo, akisema matukio hayo yanaibua wasiwasi kuhusu usalama wa wananchi.
Amesema kuvurugwa kwa mikutano ya amani na kuendelea kwa vitendo vya kutoadhibiwa kwa wahusika ni ishara kwamba mamlaka ya sheria yanazidi kudhoofika.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

