HAALAND AONGOZA NORWAY HADI ROBO FAINALI KWA KUIBWAGA BRAZIL
Norway imeandika historia kwa kutinga robo fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya kuishangaza Brazil kwa ushindi wa mabao 2-1.
Erling Haaland aliifungia Norway mabao mawili katika kipindi cha pili, huku Brazil ikijutia penalti ya kipindi cha kwanza iliyokosa kufungwa na Bruno Guimarães.
Brazil ilipata penalti nyingine mwishoni mwa mchezo iliyofungwa na Neymar, lakini haikutosha kuizuia Norway kutinga hatua ya robo fainali.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

