AMROUCHE ATAKA AFRIKA KUKUZA VIPAJI VYA NDANI
Aliyekuwa kocha wa Harambee Stars, Adel Amrouche, amezitaka nchi za Afrika kuwekeza katika ukuzaji wa vipaji vya ndani badala ya kutegemea suluhisho za muda mfupi ili kufanikiwa katika Kombe la Dunia.
Kocha huyo raia wa Algeria amesema matokeo duni ya timu nyingi za Afrika yanatokana na kupuuzwa kwa maendeleo ya soka la vijana na mifumo ya msingi ya mchezo.
Amrouche amesisitiza kuwa mafanikio ya kudumu yatapatikana kupitia mipango ya muda mrefu, uvumilivu na uwekezaji katika kukuza wachezaji chipukizi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

