ALIYEKUWA RAIS WA LSK AKASHIFU WAHUNI WANAOVAMIA MIKUTANO
Aliyekuwa Rais wa chama cha wanasheria nchini LSK Faith Odhiambo ametoa wito kwa serikali kuchukua hatua za haraka kuwakabili wahuni na magenge ya watu wanaovamia mikutano ya kisiasa.
Katika taarifa yake Odhiambo amehusisha wezi wa kimabavu katika mkahawa mmoja eneo la westlands akitaja tukio hilo kuwa tishio kubwa kwa usalama wa kitaifa.
Haya yanajiri baada ya washukiwa saba kukamatwa kwa tuhuma za kuzua vurugu kwenye msafara wa viongozi wa vuguvugu la linda mwananchi katika kaunti ya kisii mwishoni mwa wiki jana.
Imetayarishwa na Hilda Ajema

