BUNGE LA MACHAKOS LAKABILIWA NA HATARI YA KUFUNGWA
Bunge la kaunti ya Machakos linakaribia kufungwa baada ya wawakilishi wadi kutoa tahadhari kuhusu kushindwa kwa serikali kutoa fedha za kuendesha shughuli tangu mwezi aprili 2026.
Wakati wa kikao kilichoshuhudia ghadhabu kiongozi wa wachache francis kavyu ameonya kuwa uwezo wa bunge kutekeleza jukumu lake la kikatiba la usimamizi na uwakilishi unapungua kutokana na ukosefu wa rasilimali za kimsingi.
Hata hivyo spika ann kiusya amethibitisha kuwa bunge limewasilisha ombi rasmi kwa kamati ya seneti ili kuingilia kati.
Imetayarishwa na Jones Koikai

