Wednesday, July 29, 2026

Nairobi 97.7 Western 89.3 Eldoret 92.3 Kitui 105.6 Taita 94.9 North Rift 84.7 Kibwezi 87.9

FAMILIA NYERI YALILIA KIFO CHA MTOTO SHULENI

Familia moja mjini Narumoru, Kaunti ya Nyeri, inaomboleza kifo cha mtoto wao wa miaka miwili na miezi tisa, Carlos Brown, aliyefariki akiwa shuleni.

Uongozi wa Shule ya Shalom umesema mtoto huyo aligongwa na basi la shule lilipokuwa likirudi nyuma.

Hata hivyo, familia ya marehemu imepinga maelezo hayo, ikidai yanakinzana na taarifa ya polisi, na sasa inataka uchunguzi wa kina pamoja na uwajibikaji kutoka kwa uongozi wa shule.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *