Wednesday, July 29, 2026

Nairobi 97.7 Western 89.3 Eldoret 92.3 Kitui 105.6 Taita 94.9 North Rift 84.7 Kibwezi 87.9

POLISI WAKANUSHA MADAI YA MTU KUPIGWA RISASI NYAHURURU

Huduma ya Taifa ya Polisi (NPS) imekanusha madai kwamba mtu alipigwa risasi wakati wa vurugu zilizotokea katika mkutano wa kisiasa mjini Nyahururu.

Polisi wamesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa kundi la watu lilivuruga mkutano huo kwa kurusha mawe, na kusababisha baadhi ya watu kupata majeraha madogo, lakini hakuna tukio la ufyatuaji risasi lililoripotiwa.

Kauli hiyo imejiri baada ya Gavana wa Murang’a Irungu Kang’ata kudai kuwa dereva wake, Joseph Gitau, alipigwa risasi na anaendelea kupokea matibabu hospitalini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *