ENGLAND YAIONDOA MEXICO KWENYE KOMBE LA DUNIA
Uingereeza imefuzu robo fainali ya Kombe la Dunia baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mexico katika mechi ya kusisimua iliyochezwa kwenye Uwanja wa Estadio Azteca.
Kiungo Jude Bellingham aliipa Uingereeza mwanzo mzuri kwa kufunga mabao mawili ndani ya sekunde 98 na kuiweka timu yake mbele kwa mabao 2-0 kabla ya mapumziko.
Licha ya kucheza na wachezaji 10 kwa sehemu ya mchezo na Mexico kupambana hadi mwisho, Uingereeza ilishikilia ushindi huo na kutinga hatua ya robo fainali.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

